Karibu katika KUFUNGULIWA! Tunaamini kwamba Yesu Anakuja hivi karibuni. Hivyo, mada kuu ya Siku 10 za Maombi mwaka huu ni
kumwalika Roho Mtakatifu abadilishe maisha yetu na ulimwengu wetu. Jiunge nasi tunapomtafuta Mungu kwa siku 10 za uamsho tukiongozwa na Roho Mtakatifu.
Kabla hajafa, Yesu aliwaahidi wafuasi Wake zawadi ya Roho Mtakatifu: “Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli” (Yohana 14:16, 17). Baadaye, mara kabla hajaondoka duniani na kwenda kuandaa mahali pa milele kwa ajili yetu, Yesu aliwaagiza wanafunzi Wake wasitoke Yerusalemu “bali waingoje Ahadi ya Baba,” ambayo ni ubatizo wa Roho Mtakatifu (Mdo. 1:4, 5).
Hata hivyo, zawadi hii iliyoahidiwa kwa kiasi kikubwa haijafunguliwa na watu wa Mungu. Huwa tunaizungumzia tu Zawadi hii. Tunajifunza na kuichunguza Ahadi hii. Lakini mara nyingi hatufikii hatua ya kuifungua Zawadi hii ya Roho Mtakatifu.
Bila ya shaka, ni Roho Mtakatifu pekee anayeweza kuifanya upya mioyo yetu yenye dhambi: “Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu” (Ezekieli 36:26).
Ni Roho Mtakatifu pekee anayeweza kubadilisha watoto wetu: “Nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu a yao utakaowazaa” (Isaya 44:3).
Pia ni Roho Mtakatifu tu anayetuunganisha na familia ya Mungu mbinguni: “Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu” (Warumi 8:16).
Lililo bora zaidi, Mungu yuko tayari kutupatia Roho Mtakatifu: “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?” (Luka 11:13).
Ahadi ipo tayari, ikitusubiri tuidai. Ellen White anaandika, “Kama wote wangekuwa na nia hiyo, wote wangejazwa kwa Roho. Popote ambapo hitaji la Roho Mtakatifu, linachukuliwa kuwa jambo lenye uzito mdogo, kumeonekana kuwa na ukame na giza la kiroho, kushuka kwa hali ya kiroho na kifo.” Anauliza pia, “Kwa kuwa hii ndiyo njia pekee tunayoweza kupokelea nguvu, kwa nini hatuhisi njaa na kiu ya karama ya Roho? Kwa nini hatuzungumzii, wala kuomba ama kuhubiri habari za Roho Mtakatifu?” (Matendo ya Mitume, Sehemu ya Kwanza, uk. 40).
Roho Mtakatifu aliye ndani yetu anatujaza upendo wa Baba na kutuwezesha kuwa mashahidi wasio na hofu na wa kufaa kwa ajili ya Kristo. Kwa nini usiombe kwa ajili ya Zawadi hii?
Tazama Ardhi Ikitetemeka
Katika 1 Samweli 14 tunapata kisa cha kusisimua cha Yonathani na mbeba silaha wake. Wakati baba yake, Mfalme Sauli, alipokuwa chini ya mkomamanga akiwa hafanyi chochote, Yonathani na mbeba silaha wake walitoroka kutoka katika eneo lao salama kuelekea katika utukufu wa Mungu. Jeshi la Wafilisti lilikuwa likiitisha Israeli; sasa jeshi lao kubwa lilikuwa limepiga kambi ng’ambo ya korongo refu, likisubiri kupigana na Israeli.
Wakisukumwa na imani yao kwa Mungu, Yonathani na mbeba silaha wake walisombera wakishuka kwenda chini korongoni na kisha wakapanda juu ya miinuko ng’ambo
ya pili ili kukabiliana na jeshi la adui peke yao. Bila hofu, mashujaa hawa wawili, walikabiliana na Wafilisti kwa nguvu za Bwana. Walipigana na kikosi kizima cha askari Mungu mwenyewe akiingilia kati. Biblia inasema “tetemeko la Mungu” lilitetemesha kambi, shamba na watu wote [1 Samweli 14:15, (Tafsiri Sisisi ya Young)]. Imani ya Yonathani ndiyo iliyompa Mungu sababu ya kufanya ardhi itetemeke mbele ya hawa mashujaa wawili. Kama Mungu asingeingilia kati kwa kutoa tetemeko la ardhi, Yonathani na mbeba silaha wake wangeshindwa kirahisi.
Mungu bado anatenda duniani leo. Jiunge nasi tunapoomba, “Ee Mungu, ni nini kitakachokupa sababu, siku 10 mfululizo, kufanya ardhi itetemeke?”
Miaka elfu mbili iliyopita, takribani waumini 120 walikusanyika kwenye chumba cha ghorofa ya pili ya nyumba juu ya mitaa iliyosongamana ya Yerusalemu. Walithubutu kuamini ahadi ya Yesu ya Roho Mtakatifu. Walithubutu kuitii amri ya Yesu ya kuingojea Zawadi hii (Mdo. 1, 2).
Hivyo walikusanyika, wakasubiri. Roho Mtakatifu alipomiminwa wakati wa Pentekoste, waumini walifunguliwa kuwa mashahidi hai wa Mwokozi aliyefufuka, Yesu Kristo! Walizipenda familia zao na familia ya imani kuliko wakati wowote uliopita. Walitoa kwa kujitolea zaidi ya walivyofanya hapo kabla. Walisimama na kuthubutu kusema habari za Kristo kuliko wakati wowote hapo kabla.
Roho Mtakatifu anapenda kufanya kazi kutoka ndani kwenda nje! Tunakukaribisha upate uzoefu wa Siku 10 za Maombi si kama utaratibu tu, bali kama mtindo mpya wa maisha.
KUFUNGULIWA! ina sehemu tatu kila siku:
Wakati wa Pekee Pamoja na Mungu
Kila siku ya siku 10 za maombi; anza kwa maombi binafsi na kusoma Biblia.
Wanafamilia/Marafiki
Tumia muda kukusanya familia yako au mzunguko wa marafiki kwa ajili ya maombi ya kila siku.
Familia ya Kanisa
Jiunge na familia yako ya kanisa kwa ajili ya kipindi cha maombi yenye vizazi tofauti kila siku.
Kusanya marafiki, washiriki wa kanisa, wafanyakazi wenzako, vijana na watoto wa rika zote kwa siku 10 za uamsho wa kiroho. Ni wakati wa kufunguliwa kikamilifu na Roho Mtakatifu tena!
Mwongozo wa Kiongozi – KUFUNGULIWA!
Kila siku ya siku 10 za Maombi itajumuisha sehemu tatu:
Wakati wa Pekee Pamoja na Mungu (Ibada Binafsi)
Furahia sehemu hii kila siku, wakati wa peke yako pamoja na Mungu. Kila mtoto anayeweza kusoma, kila kijana na kila mtu mzima anaalikwa kukutana na Mungu katika Neno lililoandikwa, kuomba na kutembea pamoja na Yesu.
Wanafamilia/Marafiki (Ibada ya Familia)
Alika familia yako au rafiki zako kutumia muda pamoja na wewe. Yeyote unayemhesabu kama mwanafamilia na awe sehemu ya muda huu. Waombee kwanza, kisha wakusanye kwa ajili ya wakati huu wa thamani katika Neno la Mungu na maombi.
Familia ya Kanisa (Mkusanyiko wa Kila Jioni) Karibisha kanisa lako, majirani na jumuiya ya marafiki kukusanyika mara moja kila siku kwa ajili ya maombi haya na shughuli hizi. Omba kwa dhati ili Mungu akuoneshe nani umwalike ili kuongeza washiriki walio hai kanisani kwako. Tafakari kwa maombi namna ya kuwaalika wewe binafsi washiriki wasio hai, washiriki wa zamani, wale uliosoma nao, wafanyakazi wenza na viongozi wa kidini wa madhehebu mengine.
Kanuni za Kufanya katika Siku 10 za Maombi Ziwe kwa Ajili ya Vizazi Changamano
Kikundi chetu cha maombi watakutana na kupanga maombi ya watu wawili ili kuomba kwa ajili ya kila mtoto, kijana na mtu mzima kwa kumtaja kwa jina kila siku. Ikiwezekana tutawaombea kwa miezi kadhaa kabla ya kuanza siku 10 za maombi. Tutatoa
nafasi kwa watu wawili wawili kuomba kwa ajili ya watu 10 kwa kutaja majina yao kabla na wakati wa siku 10 za maombi. Tutaomba kwamba Roho Mtakatifu aandae kila moyo kulipokea Neno la Mungu lililoandikwa na kufunguliwa Naye.
Tutatumia Neno la Mungu lililoandikwa kama mwongozo wetu wa msingi. Tutafanya kila linalowezekana kwa ajili ya upatikanaji wa Biblia kwa watu wazima wote na watoto wanaoweza kusoma. Pia kila siku tutabarikiwa kwa maneno yenye kuleta msukumo kutoka kwa Ellen G. White.
Wale tunaojitolea kualika familia ya Kanisa ili kuomba, tutajitolea kwanza katika:
Kutenga kila siku wakati wa pekee pamoja na Mungu katika maombi na Neno Lake.
Kujisalimisha kwa Yesu kama Bwana
Kuomba na kupokea kwa imani ubatizo wa Roho Mtakatifu.
Tutajumuisha kila rika katika vikundi vidogo vyenye watu sita au pungufu ya hapo vikiongozwa na mwanafunzi mmoja na mtu mzima mmoja kwa ajili ya kila mkutano wa familia ya Kanisa.
Tutachagua hawa viongozi wa vikundi hivi vidogo (wawili kwa kila kikundi: mtu mzima mmoja na mtoto/kijana mmoja) kwa maombi ya dhati na kumngojea Mungu na kuwaandaa viongozi hawa kuongoza watu wao kama wanaowafanya kuwa wanafunzi.
Tutajumuisha rika zote kadiri inavyowezekana katika kila sehemu ya kuongoza Maombi haya ya Siku 10 na tutajitahidi kufanya kila sehemu ieleweke kwa mtoto mwenye umri wa miaka 10.
Tutafanya maombi yetu kuwa mafupi ili kila mtu katika kikundi chetu aweze kushiriki. Mara nyingi, ombi la sentensi moja au mbili linatosha na kufanya wakati huu uwe wenye kuvutia kwa ajili ya watoto na vijana.
Tutajitahidi kuongoza kila mtu katika kushiriki kwa vitendo katika Siku 10 za Maombi, kuliko kuwa mtazamaji.
Tutaimba nyimbo zenye kuleta tafakari kwa rika zote na kusaidia kila mtoto, kijana na mtu mzima kujua kuwa wanayo sauti katika ibada.
Tutasalimisha mipango yetu ya kila mkutano kwa uongozi wa Roho Mtakatifu.
Tutatoa chakula chepesi cha jioni kabla ya kila mkutano wa familia ya Kanisa ili kuutia moyo ushirika wa waumini kama ilivyo katika kitabu cha Matendo ya Mitume (taz. Mdo. 2:42).
Namna ya Kuongoza Siku 10 za Maombi kwa Ajili ya Matokeo Makubwa
Siku kumi kabla ya Siku 10 za Maombi kuanza: Soma na kuomba katika sehemu zote za mwongozo wa kila siku: Wakati Pekee Pamoja na Mungu, Wanafamilia/ Marafiki na Familia ya Kanisa.
Wakati wa Siku 10 za Maombi: Soma na kuombea mwongozo wa kila siku tena. Tunatumaini, wewe binafsi utapitia uzoefu wa nguvu ya Neno la Mungu likiambatana na Roho Mtakatifu kabla ya kulialika kanisa lako kufanya vivyo hivyo.
Hakikisha Muda Pekee Pamoja na Mungu na Familia/Rafiki unapatikana kila siku kwa kila mtu anayehudhuria kipindi cha jioni cha Familia ya Kanisa.
Kwa ajili ya Familia ya Kanisa kila siku:
Omba pamoja na viongozi wote wa vikundi vidogo, viongozi wa maombi na viongozi wa nyimbo dakika 30 kabla ya kipindi kuanza.
Elekeza vikundi vidogo vyote kutoka mbele kwa
ajili ya maombi na maelekezo kutoka kwenye Neno ili vikundi hivyo vianzishwe na viunganishwe katika maombi na kujifunza Neno.
Jipatie changamoto ya Saa 24 wewe mwenyewe
ya kufuata mambo haya kila siku ili uwe mkweli unapouliza kila mtu alifanya nini katika changamoto hiyo siku inayofuata.
Kwa maombi mengi, shiriki wito pendekezwa
kutoka moyoni mwako. Usiusome. Omba na wale wanaoitikia na wale wasioitikia.
Jiandae kushiriki ushuhuda wako mwenyewe
kuhusu jinsi kifungu cha Maandiko cha kila kipindi kinavyoathiri maisha yako. Toa ushuhuda wako kabla ya wito—ukionesha nguvu ya Kristo ya kubadilisha maisha kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, si kwa nguvu zako binafsi.
Funga mkutano kwa kumshukuru kila mtu kwa
kuwa sehemu ya kile ambacho Mungu anafanya katika Siku 10 za Maombi.
Baada ya kila mkutano, jitayarishe kwa miadi ya
Kiungu na wale wenye maswali au wanaohitaji maombi.
Panga Mkutano wa “Kipi Kinafuata?” utakaofanyika mara moja baada ya Siku 10 za Maombi. Hizi siku 10 za maombi si mwisho kwa zenyewe. Roho Mtakatifu yupo tayari zaidi kufanya mikutano hii iwe kichocheo cha utume binafsi, wa kifamilia na wa familia ya kanisa katika jamii yako na ulimwenguni
kote! (Angalia muhtasari uliowekwa kwa ajili ya Mkutano wa “Kipi Kinafuata?”)
Vitu Unavyohitaji kwa Ajili ya Mikutano ya Jioni ya Familia ya Kanisa:
Eneo la mkutano lililo kubwa la kuwatosha
washiriki wote kukaa katika vikundi vidogo vya watu sita.
Kiongozi wa maombi mwenye kukubali
mabadiliko kuongoza vipindi vya Familia ya Kanisa kutokea mbele.
Wajumbe wa ziada wa timu ya maombi kupanga
na kuandaa nyimbo za wakati wa maombi ya vikundi.
Viongozi wawili (mtu mzima mmoja na kijana
mmoja) kwa kila kundi dogo lenye watu sita.
Biblia kwa washiriki wote (wanaweza kuleta za kwao au mnaweza kuwapatia).
Nakala za mwongozo wa kila siku wa maombi
kwa washiriki (au ufikishwe kidigitali ikiwa inapendelewa).
Kwa ajili ya Mkutano wa Kipi Kinafuata?: ubao
mkubwa wa kuandikia na kuweza kufuta, kalamu maalumu, karatasi zenye gundi au karatasi/utepe.
Mtiririko Unaopendekezwa kwa Ajili ya Mikutano ya Jioni ya Familia ya Kanisa (pamoja na muda unaopendekezwa)
6:00 Chakula chepesi cha jioni
6:30 Maombi na viongozi wote wa vikundi vidogo, viongozi wa maombi na viongozi wa nyimbo
7:00 Ukaribisho (kutoka mbele kwanza kisha katika vikundi vidogo)
7:03 Ibada katika Maombi
Shukrani/Sifa (mojawapo)
Ungama/Tubu (mojawapo)
Omba
7:25 Shuhudia(shirikiana katika vikundi vyenu kile Mungu alichokusaidia kufanya katika Changamoto ya Saa 24)
7:30 Shughuli ya Kushirikiana
7:35 Ibada katika Neno (Maandiko na majadiliano) 7:45 Kusudi la Maombi
7:55 Wito/Maombi/Kushiriki Changamoto ya Saa 24 8:00 Washukuru watu kwa kuja na wape ruhusa ya
kuondoka
Machapisho ya Siku Kumi za Maombi yameandaliwa na Chama cha Wachungaji, Konferensi Kuu ya Waadventista wa Sabato. Copyright © 2025. Mchangiaji Mkuu: Don MacLafferty.
Mkutano wa Mwisho: “Kipi Kinafuata?”
Vitu Vinavyohitajika, Ikiwa Vinapatikana:
Ubao mkubwa unaoweza kufutika (dry erase board) au kitu cha kufanana, kinachoweza kugawanywa katika sehemu 4, AU mbao 4 ndogo zilizowekwa kwenye viweko.
Karatasi zenye gundi (Sticky notes, ikiwa zinapatikana) AU vipande vidogo vya karatasi na utepe vya kushikiza kwenye ubao.
Kalamu maalumu zinazoweza kufutika (Markers za dry erase) kwa ajili ya kuandikia vichwa vya kila sehemu AU karatasi, kalamu na utepe ikiwa unataka kushikiza vichwa ili kuviweka mahali pengine.
Kwa Nini?
Roho Mtakatifu amekuwa akitenda kazi katika maisha yako na kanisa lako! Fuatilia mara moja Siku 10 za Maombi kwa kuwakusanya watu wa Mungu pamoja ili kuomba na kutafuta mpango Wake. Hatari inaweza kuwa kurudi kwenye taratibu za zamani na kupoteza msukumo aliouunda Mungu katika siku hizi za maombi yanayobadilisha maisha. Panga kukutana pamoja haraka iwezekanavyo!
Ni Kitu Gani?
Mkutano huu ni kwa ajili ya kutafuta kile Mungu anachotuita kukifanya katika maeneo manne:
Eneo binafsi
Eneo la wana Familia/Marafiki
Familia ya Kanisa
Eneo la jamii pana/Ulimwengu
Kwa Namna Gani?
Hapa kuna pendekezo moja la namna ya kuendesha mkutano. Mwombe na kumsihi Mungu akusaidie kuongeza au kupunguza chochote katika muhtasari huu kulingana na kanisa lako.
Muhtasari wa Kipindi cha Mwisho
Mkutano unapoanza, ketisha familia au wanandoa pamoja. Waombe wengine waunde vikundi vidogo ya marafiki, ikihakikishwa kila mtu anashirikishwa. Uwe na viongozi walio tayari kusaidia kujumuisha kila mtu katika kikundi.
Ukaribisho na Maombi Shughuli ya Kushirikiana
KIONGOZI KWA WOTE: Jadili maswali yafuatayo na kundi la familia/marafiki:
Taja tukio moja maishani ambalo ulijisikia kuwa umejiandaa kwalo zaidi.
Kisha, taja tukio moja maishani ambalo ulijisikia kutojiandaa vya kutosha kwalo.
Kumwabudu Mungu kwa Shukrani (WOTE)
Imba wimbo wa shukrani na kundi lote.
Waalike wanaojitolea kushiriki kile Yesu Kristo alichofanya katika maisha yao wakati wa Siku 10 za Maombi.
Imba wimbo mwingine wa shukrani pamoja.
Mtu mmoja aombe kwa ajili ya ujio wa Roho Mtakatifu ili kuongoza mkutano huu.
Mtu mmoja asome Waefeso 3:20, 21 kwa kundi lote. Aya hii inapaswa kuathiri vipi kanisa tunapojitayarisha kwa kile kinachofuata? Waalike washiriki kushiriki mawazo yao.
Weka ubao mkubwa ulio na sehemu 4, (au uweke mbao 4 ndogo mbele ya kila mtu ili aone). Tambua sehemu nne: BINAFSI, FAMILIA/MARAFIKI, FAMILIA YA KANISA, JAMII/ULIMWENGU.
KIONGOZI KWA WOTE: Tunamwomba Mungu atuoneshe hatua maalumu za kuchukua katika maeneo haya manne. Si mawazo ya jumla, bali yale yaliyo mahususi na yanayoweza kupimika. (Mfano: SI “Kuwa vizuri zaidi kiroho,” bali,“ kuwa na wakati wa pekee usioingiliwa wa kuwa pamoja na Mungu katika Neno Lake na maombi KABLA ya kifungua kinywa kila siku.”)
Binafsi
Mpatie kila mtu karatasi za gundi na kalamu. Jumuisha rika zote.
Waalike watu wote kuwa na muda wa kuomba kimya. Mwombe Mungu kwa kitu kimoja ambacho anakuita kufanya kama hatua binafsi katika uamsho wako pamoja na Yesu.
Andika kwa ufupi kwenye karatasi sentensi moja au neno moja. Waalike washiriki kugundisha karatasi kwenye sehemu ya “Binafsi.” (Pia wanaweza kuzitunza.)
Wanafamilia/Marafiki
Toa karatasi moja yenye gundi kwa kila kundi la familia/marafiki.
Waalike kuomba pamoja. Wamwombe Mungu kitu kimoja ambacho kitasaidia familia au kanisa kukua na kupata mwamko wa kila siku.
Jadili.
Andika kwa ufupi na bandika kwenye sehemu ya “Familia / Marafiki.”
Familia ya Kanisa
Waombe washiriki wagawanyike na kuunda vikundi vidogo vidogo vyenye watu 6 au pungufu katika Siku 10 za Maombi. (Ikiwa washiriki wapya hawapo katika kundi lolote, wagawe kuwa sehemu ya vikundi vilivyopo.)
Alika vikundi vidogo kuomba pamoja. Wamwombe Mungu kitu kimoja ambacho kitaisaidia familia ya kanisa kupata uzoefu wa uamsho wa kila siku pamoja na Yesu.
Jadili.
Andika “kitu kimoja” na bandika kwenye sehemu ya “Familia ya Kanisa.”
Jamii/Ulimwengu
Toa karatasi nyingine yenye gundi kwa kila kundi dogo.
Waalike kuomba. Wamwombe Mungu awafundishe njia moja ya kuifikia jamii na ulimwengu kwa habari njema ya Yesu. Fikiria kitu cha wakati huu na kinachohusiana.
Jadili.
Andika “kitu kimoja” kwa sentensi moja na bandika kwenye sehemu ya “Jamii/Ulimwengu.”
(WOTE)
Tengeneza mduara na mwombe Mungu azibariki hatua hizi zinazofuata.
Waambie washiriki wa Siku 10 za Maombi kwamba wachungaji au wazee wa kanisa watachunguza maoni haya, kuyaombea na kutoa mapendekezo katika baraza la kanisa na washiriki kuhusu hatua zinazofuata ambazo kwa pamoja na Kanisa mnaweza kuzipiga. Kwa pamoja jitahidini kuishi maisha mapya ya maombi. Hebu mtazame Roho wa Mungu anapokuwa akifunguliwa kwa nguvu nyumbani kwako na kanisani kwako!

Prayer
Claim Psalm 119:105 in prayer. Ask God to send the Holy Spirit to make the written Word a light for your faith walk.
Explore the Word
- Read Acts 1:1–3. What does this passage teach you about Jesus?
- Explore the four Gospels to see how many times Jesus revealed Himself ALIVE to His followers after His resurrection. (See Matt. 28:9–20; Mark 16:9–20; Luke 24:13–53; John 20:14 to 21:25.)
Insights from Ellen White:
For forty days Christ remained on the earth, preparing the disciples for the work before them and explaining that which heretofore they had been unable to comprehend. He spoke of the prophecies concerning His advent, His rejection by the Jews, and His death, showing that every specification of these prophecies had been fulfilled. He told them that they were to regard this fulfillment of prophecy as an assurance of the power that would attend them in their future labors. “Then opened He their understanding,” we read, “that they might understand the Scriptures, and said unto them, Thus it is written, and thus it behooved Christ to suffer, and to rise from the dead the third day: and that repentance and remission of sins should be preached in His name among all nations, beginning at Jerusalem.” And He added, “Ye are witnesses of these things.”
During these days that Christ spent with His disciples, they gained a new experience. As they heard their beloved Master explaining the Scriptures in the light of all that had happened, their faith in Him was fully established. They reached the place where they could say, “I know whom I have believed.” 2 Timothy 1:12. They began to realize the nature and extent of their work, to see that they were to proclaim to the world the truths entrusted to them. The events of Christ’s life, His death and resurrection, the prophecies pointing to these events, the mysteries of the plan of salvation, the power of Jesus for the remission of sins—to all these things they had been witnesses, and they were to make them known to the world. They were to proclaim the gospel of peace and salvation through repentance and the power of the Saviour. (The Acts of the Apostles, pp. 26, 27)